HUJAMBO

"KARIBU UJIUNGE NASI KUPATA TAARIFA MBALIMBALI ZA MICHEZO YA VYUO VIKUU KILA SIKU KUTOKA HAPA NCHINI TANZANIA HIZI NI HABARI ZA MICHEZO AMBAZO ZIMEVIHUSU VYUO VYA HAPA NCHINI IKIWA NI PAMOJA NA USHIRIKI WA VYUO KATIKA MATAMASHA MBALIMBALI KITAIFA NA KIMATAIFA MABONANZA NA MASHINDANO MAKUBWA YA KIMATAIFA YANAYO HUSU VYUO VIKUU, KUMBUKA MICHEZO HUANZIA MASHULENI NA KATIKA VYUO MUENDELEZO NDIKO UNAKOPATIKANA KARIBU SANA"

Thursday, March 22, 2012

WASIFU WA MAREHEMU ANDREA LESSO HANGE (25/12/1970 – 01/03/2012)




 Kuzaliwa                         25/12/1970
Katesh – Manyara Zamani Arusha

Shule ya Msingi                 1977-1983
Sambaru Shule ya Msingi  iliyoko Singida

Elimu ya Sekondari            1984-1987
Tumaini Shule ya Sekondari-  (Singida)
Kidato cha kwanza hadi cha nne

1988-1990 Shule ya Sekondari Sengerema - Mwanza
Kidato cha tano na cha sita

1990                               Alijiunga na jeshi la kujenga taifa kwa mujibu wa sheria (Makuyuni JKT -Arusha)

1991-1993                       Mwaka 1991 Marehemu alichaguliwa kujiunga na Chuo cha Ualimu Marangu na kuhitimu stashahada ya Ualimu mwaka 1993

1993                               Aliajiriwa kufundisha shule ya Sekondari Siha iliyoko Mkoani Kilimanjaro. Alifanya kazi mpaka 1995.

11/12/1994                      Tarehe 11/12/1994 Alifunga NDOA Takatifu na Bi Dianaeli G. Masaki katika kanisa la TAG Sayuni – Sanya juu
                  

1995 -1999                      Mwaka 1995 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salaam, na kuhitimu  digrii yake ya kwanza ya elimu ya Viungo, Michezo na Utamaduni (Physical Education, Sports and Culture) mwaka 1999.

1999-2002                       Mwaka 1999 alipata nafasi ya kuendelea na masomo Chuo Kikuu cha Dar es salamm akisoma digrii ya pili ya Elimu (M.A Education) na alihitimu mwaka 2002

2002                               Mwaka 2002 Aliajiriwa na Chuo Kikuu cha Dar es salaam kama Mkufunzi Mkuu wa Michezo akiwa chini ya ofisi ya Mshauri wa wanafunzi, Aidha akiwa anashughulika na shughuli za michezo, marehemu pia alikaimu nafasi ya afisa tawala Ofisi ya Mshauri wa wanafunzi hadi mwaka 2005.

2006                               Mwaka 2006 Marehemu alibadilishwa kazi kutoka kazi ya -Ukufunzi wa Michezo na alijiunga na Idara ya Elimu ya Viungo na Sayansi za Michezo  chini ya Shule Kuu ya Elimu ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam akiwa Mhadhiri Msaidizi yaani Assistant  Lecturer cheo ambacho amedumu nacho hadi mauti yanampata.

2011                               Novemba 2011, Alijiunga na Chuo Kikuu cha Kristianstad Kilichopo Swedeni kwa ajili kumalizia masomo yake ya PhD aliyoyaanza mwaka 2005  Chuo Kikuu Huria.


USHIRIKI WA MAREHEMU KATIKA MICHEZO

1981 -1983-                     Marehemu alishiriki katika mashindano ya Mbalimbali. Alishiriki mashindano ya UMITASHIMUTA kwa ngazi ya Taifa  akiwa mshiriki katika mchezo wa mpira wa miguu na riadha akiwa shule ya Msingi.

1985 -1991                      Akiwa shule ya Sekondari Marehemu alishiriki kwenye michezo ya UMISSETA akiwa mchezaji wa mpira wa miguu, riadha na mpira wa wavu akiwakilisha kanda ya kati.
                                      Marehemu alishiriki kwenye michezo ya UMISSETA kanda ya ziwa akiwa mshiriki katika michezo ya soka na wavu ( Shinyanga na Tabora)

1991                               Akiwa Jeshini Marehemu alishiriki Michezo ya Majeshi iliyofanyika Arusha akiwa anacheza mpira wa miguu.

1992-1993                       Alichezea timu ya USHIRIKA mkoani Kilimanjaro ikiwa daraja la kwanza.

1996-                              1998 Akiwa mwanafunzi wa chuo kikuu alishiriki katika michezo ya SHIMIVUTA na kukiwakilisha Chuo katika michezo mbalimbali .

2003                               Mwaka 2003 alishiriki michezo ya SHIMMIVUTA iliyofanyika Arusha akiwa Kocha Mkuu wa timu ya Chuo Kikuu cha Dar es salamm.

2002-2004-2006.             Alikua Kocha mkuu wa timu ya chuo kikuu cha Dar es salaam iliyoshiriki kwenye michezo ya Vyuo vikuu vya Afrika Mashariki. Iliyo fanyika UDSM, Kenyatta University na Kampala University.

2007                               Mwaka 2007 alishiriki Michezo ya Vyuo Vikuu vya Dar es salaam akiwa Kocha Mkuu wa timu ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Tangu 2008-                    Amekuwa mwamuzi wa mashindano mabali mabali ya Shirkisho la Riadha nchini

2010                               Alihudhuria, na kufaulu, mafunzo ya ufundishaji (kocha) wa riadha ya vijana kwenye Kituo cha Maendeleo ya Riadha cha Shirikisho la Duania la Riadha kilichopo Nairobi.

January, 2012                  Alichaguliwa kuwa mjumbe wa Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam

                                                               
NAFASI NMBALIMBALI ALIZOSHIKA MAREHEMU

1997-1998                       Alikua Mweka Hazina wa Shirikisho la Michezo ya Vyuo Vikuu Tanzania (TUSA).

2002-2004                       Alikua ni Kocha Mkuu na Mratibu wa shughuli za michezo Chuo kikuu cha Dar es salaam

2003- 2004                      Mwakilishi wa Wafanyakazi wa ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi katika Baraza la Wafanyakazi la Chuo Kikuu cha Dar es salaam

2005                               Hadi mauti yanampata alikua Katibu Mkuu Msaidizi kwenye Shirikisho la Michezo ya Vyuo Vikuu Tanzania (TUSA).

2011 -                             Pia hadi mauti yanampata Marehemu alikuwa Mjumbe wa Halmashauri kuu wa THTU – Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Mwakilishi wa Tawi katika Halmashauri ya THTU taifa.


HUDUMA KWA JAMII

Marehemu amekua akishiriki katika uandaaji wa matamasha mbalimbali ya michezo ya wafanyakazi, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam pamoja na mashirika mengine ya umma na binafsi.
                                    
Marehemu alijihusisha sana na wanafunzi wenye ulemavu mbalimbali kwenye suala la michezo, na hilo ndilo lilimpa hamasa ya kwenda kusoma PHD inayohusiana mambo ya ulemavu




MAREHEMU AMEACHA MKE NA WATOTO WAWILI.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA,
JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.


No comments:

Post a Comment